127 – Nisalama Rohoni Mwangu

0
40

127. Nisalama Rohoni Mwangu
When Peace Like A River

1. Nionapo amni kama shwari, au nionapo shida;
Kwa hali zote umenijulisha ni salama rohoni mwangu.

Salama rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

2. Ingawa Shetani atanitesa, nitajipa moyo kwani,
Kristo ameona unyonge mwangu; amekufa kwa roho yangu.

3. Dhambi zangu zote, wala si nusu, huwekwa msalabani;
Wala sichukui laana yake, ni salama rohoni mwangu.

4. Ee Bwana himiza siku ya kuja, panda itakapolia:
Utakaposhuka sitaogopa ni salama rohoni mwangu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here