128 – Taamini Nitii Pia

0
36

128. Taamini Nitii Pia
When We Walk with the Lord

1. Namwandama Bwana kwa aliloneno,
Njia zangu huning’azia;
Na nikimridhisha atanirudisha,
Taamini nitii pia.

Kuamini, Njia pweke ni hii
Ya furaha kwa Yesu: Amini ukatii.

2. Giza sina kwangu wala hata wingu,
Yeye mara huviondoa;
Oga, wasiwasi, sononeko, basi;
Huamini nitii pia.

3. Masumbuko yote, sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia;
Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki.
Taanimi nitii pia.

4. Mimi sitajua raha sawasawa
Ila yote Yesu kumtoa:
Napata fadhili na radhi kamili,
Taamani nitii pia.

5. Nitamfurahia na kumtumaini,
Majumbani na njia-njia;
Agizo natenda; nikitumwa hwenda,
Huamini, nitii pia.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here