163 – Anakuja, Bwana Yesu

0
41

163. Anakuja, Bwana Yesu
It May Be A Morn

1. Pengine ni saa ya kupambazuka, Mishale ya jua ipenyapo giza,
Kwamba atakuja Yesu mtukufu, Awapokee wake.

Bwana itakuwa lini Tutapoimba
“Anakuja, Bwana Yesu, Aleluya, Amin, Aleluya, Amin?”

2. Pengine mchana, pengine jioni, Pengine usiku wa manane, giza
Itatoweka kwa fahari akija, Awapokee wake.

3. Majeshi yake yataimba “Hosana,” Na watakatifu waliotukuzwa
Watamsifu kwa kuwa amekuja Awapokee wake.

4. Furaha tukiitwa pasipo kufa, Pasipo kuona maradhi, machozi;
Kuchukuliwa winguni kwa fahari Akija kwa watu wake.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here