74 – Niambie, Ee Mlinzi

0
53

(NZK # 74) NIAMBIE, EE MLINZI
Watchman, Tell Me

1. Niambie, Ee Mlinzi, Umepambazuka Je!
Utukufu Wa Zayuni; Pana Dalili Zake?
Msafiri Uondoke, Utazame Mbinguni,
Kiunoni Ujifunge, Ni Kucha, Alifajiri.

2. Mlinzi, Inamulika Nuru Njiani Mwako,
Dalili Ya Kuja Kwake, Kwamba Siku Karibu;
Panda Itakapolia Itawaamsha Wafu,
Watakatifu Wa Mungu, Kuwapa Kutokufa.

3. Mlinzi, Ione Nuru Ya Mwaka Wa Sabato;
Sauti Zina Tangaza Ufalme Ni Karibu:
Msafiri Ninaona Mlima Wa Zayuini,
Mji Wa Yerusalemu Nayo Fahari Yake.

4. Kwenye Mji Wa Dhahabu Anaketi Mfalme
Katika Kiti Kizuri: Huku Ana Tawala.
Pana Amani Po Pote, Mashamba Husitawi;
Na Ardhi Ina Rutuba; Mito Ni Mitulivu.

5. Mlinzi, Twakaribia Nchi Iliyo Nzuri;
Twende Mbele, Tufurahi, Nchi Inachangamka.
Sikieni Kuna Wimbo Wa Waliookoka;
Kaza Mwendo, Ujiunge Na Kundi Kubwa Hili.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here