137 – Saa Heri Ya Sala

0
41

137. Saa Heri Ya Sala
‘Tis the Blessed Hour of Prayer

1. Saa heri ya sala tunapojidhili,
Kama tukija kwake yesu rafiki.
Tukiwa na imani kwamba yu mlinzi,
Waliochoka sana watapata raha.

Saa ya sala, iliyo heri;
Waliochoka sana watapata raha.

2. Saa heri ya sala, ajapo mwokozi,
Ili awasikie watoto wake.
Hutwambia tuweke miguuni pake
Mizigo yetu yote: tutapata raha.

3. Saa heri ya sala, wawezapo kuja
Kwa Bwana Yesu wanaojaribiwa;
Moyo wake mpole, atawarehemu;
Waliochoka sana watapata raha.

4. Saa heri ya sala tutakapopewa
Mibaraka ya roho, tukimwamini;
Kwa kuamini kweli hatutaogopa;
Waliochoka sana watapata raha.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here