155 – Njiani Huniongoza

0
40

155. Njiani Huniongoza
All the Way my Saviour Leads Me

1. Njiani huniongoza. Yesu wangu, Mwokozi;
Rehema hatapunguza, Milele Kiongozi.
Ina raha kwandamana Duniani daima;
Nijaposumbuka sana, Yeye hutenda vyema,

2. Njiani huniongoza Hupunguza matata;
Nikiugua hupoza, Na njaani nashiba.
Lichokapo guu langu Nguvu zikapungua,
Jiwe lilo mbele yangu Hunibubujikia.

3. Njiani huniongoza Kwa pendo zilizo kuu,
Mwisho atanituliza Kwake Baba yangu juu.
Nikivikwa kutokufa, Nikae na Mwokozi,
Nitamsifu sana; sifa: “Kweli ni Kiongozi.”

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here